
Dk. Mohammed Gharib Bilal Aaanza Kazi Ramsi November 08, 2010
MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Mohammed Gharib Bilal, amewataka watumishi wa ofisi yake kujizatiti katika utekelezaji wa majukumu yao. Amesema kwa kufanya hivyo, watawezesha kupatikana mafanikio katika awamu ya pili ya uongozi wa Rais Jakaya Kikwete. Dk. Bilal alisema hayo alipozungumza na Menejimenti ya ofisi hiyo. Alisisitiza umuhimu wa watendaji na watumishi wa ofisi hiyo kufanya kazi kwa mujibu wa Katiba, sheria na kuzingatia taratibu za mawasiliano ya kiserikali. Dk. Bilal aliwakumbusha kufanya kazi kama timu moja ya serikali na nchi moja. Alisema anatarajia kuona wanajituma kwa kuzingatia misingi ya utawala bora, uwazi na kuendeleza heshima ya ofisi.
Ningependa kuona system (mfumo) inafanya kazi inavyotakiwa, utendaji rasmi unaoheshimu mtu na nafasi yake. Ninaamini sote tutajitahidi kufanya kazi kwa mujibu wa Katiba, Sheria na taratibu zilizowekwa,î alisema. Aliwakumbusha watumishi hao wajibu wa kuelewa mfumo mzima wa utendaji wa serikali, ili aweze kufanikisha majukumu yake ya kumsaidia Rais Kikwete. Makamu wa Rais aliwaasa watumishi kuzingatia wadhifa, fursa na wajibu waliopewa katika kuendeleza maelewano mazuri yaliyopo katika ofisi hiyo.
Dk. Bilal alisema majukumu ya wizara za Muungano na Mazingira zilizo chini ya ofisi yake ni muhimu kwa mustakabali wa taifa, hivyo hawana budi kuwa makini katika utekelezaji wa majukumu kwa kuzingatia ujuzi, taaluma na uzoefu wao. Kwa upande wake, Katibu Mkuu, Ofisi ya Makamu wa Rais, Ruth Mollel, aliahidi kufanya kazi kwa kuzingatia taratibu, sheria na utawala bora.
Aidha, Dk. Bilal alibainisha kuwa majukumu ya wizara mbili katika ofisi hiyo yaani za Muungano na Mazingira ni muhimu kwa mustakabali wa taifa na hivyo hawana budi kuwa makini katika utekelezaji wake huku wakizingatia ujuzi wao, taaluma na uzoefu wao.
“Mazingira ni suala muhimu, yanatugusa sote popote tulipo, hivyo, tunapaswa kuwa makini zaidi. Nchi yetu ni changa hatuwezi kukabiliana na changamoto zinazotokana na athari za mazingira.
Tuimarishe ujuzi wetu, uelewa wetu na uzoefu wetu katika suala hili hapa petu na kwa jirani zetu na kwingineko,” alifafanua.
Dk. Bilal aliwakumbusha watumishi wa ofisi hiyo wajibu wao wa kuelewa mfumo mzima wa utendaji wa serikali ili afanikishe majukumu yake ya kumsaidia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Dr. Mohammed Gharib Bilal - Wengi Wamerudi CCM Jee Wewe?

Dr. Kikwete : Arejea Tena Ikulu
MWENYEKITI wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, ( NEC), Jaji Mstaafu, Lewis Makame amemtangaza mshindi wa kiti cha urais wa Tanzania wa mwaka 2010 kuwa ni Dk. Jakaya Kikwete kutoka Chama cha Mapinduzi(CCM).
Matokeo hayo ya uchaguzi huo, yalitangazwa 05/11/2010 majira ya saa kumi jioni na Mwenyekiti huyo katika viwanja wa Karimjee jijini Dar es Salaam.
Kabla ya kutangazwa kwa matokeo hayo, Jaji Mstaafu , Makame alisema kwa mujibu wa Ibara ya 41(6) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, mwaka 1977 mgombea wa kiti cha urais atatangazwa kuwa amechaguliwa kuwa rais iwapo tu amepata kura nyingi kuliko mgombea mwingine yeyote.
Aidha Makame alisema kwa mujibu wa ibara ya 47(2) ya Katiba hiyo, mgombea wa kiti cha urais akichaguliwa basin a mgombea mwenza wake atakuwa Makamu wa Rais.
“Kwa kuwa Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete wa CCM amepata kura yingi kuliko mgombea yeyote, kwa niaba ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi na kwa mujibu wa vifungu vya 35E, 35F (8) na 81 B vya Sheria ya Taifa ya Uchaguzi Sura 343, ninatangaza rasmi matokeo ya uchaguzi wa urais wa 2010.
“Mheshimiwa Kikwete Jakaya Mrisho amechaguliwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mheshimiwa Bilal Mohammed Gharib amechaguliwa kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,” alisema Mwenyekiti huyo.< br />
Aliongeza kuwa idadi ya wapigakura waliojiandikisha ni 20,137,303, waliopiga kura ni 8,626,283 sawa na asilimia 42.84 ya wapiga kura wote waliojiandikisha, zilizoharibika ni 227,889 ambazo ni sawa na asilimia 2.64 ya kura zilizopigwa.
Alizitaja idadi ya kura halali kuwa ni 8,398,394 sawa na asilimia 97.36 ya kura zote zilizopigwa, hivyo Kikwete amepata kura 5,276,827 ambazo ni sawa na asilimia 61.17 ya kura zote halali.
Wagombea waliofuatia ni wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA) ambaye ni Slaa Willibrod Peter amepata kuwa 2,271,941 ambazi ni sawa na silimia 26.34 ya kura zote halali, Lipumba Ibrahim Haruna wa chama cha CUF, amepata kura 695,667 sawa na asilimia 8.06 ya kura zote halali, Mziray Kuga Peter wa APPT – Maendeleo amepata kura 96,933 sawa na asilimia 1.12 ya kura zote halali.
Wengine ni Rungwe Hashim Spunda wa NCCR- MAGEUZI amepata kura 26,388 sawa na asilimia 0.31 ya kura zote halali, Mgaywa Muttamwega Bhatt wa TLP amepata kura 17,482 sawa na silimia 0.20 na Dovutwa Yahmi Nassoro Dovutwa wa UPDP amepata kura 13,176 sawa na asilimia 0.15 ya kura zote halali.
Akitoa salamu kwa niaba ya wenzake badala ya Slaa ambaye hakuwepo uwanjani hapo, Lipumba alimpongeza Kikwete na Makamu huku akisisitiza suala ya ushiriki wa watu katika kupiga kura liangaliwe na kusema Rais aliyeshinda ni Watanzania wote.
Alisisitiza suala la elimu bora , ajira, ujengaji wa miundombinu na uvumulivu wa kisiasa ni muhimu, hivyo alimshauri Rais Mteule Kikwete kujiwekea malengo katika kipindi cha miaka 5 ijayo, ambayo ni uongozi wa demokrasi, ujenzi wa uchumi ajira kuboresha miunbombinu, utawala na kupamban na rushwa.
Pia alimkabidhi Rais Mteule Kikwete Ilani ya chama chake kwa ajali ya kusaidia katika utendaji wake wa kazi.
Kwa Upande wake Rais Mteule Kikwete, alitoa shukurani za ushindi alioupata na kusema watazifanyia kazi changamoto zilizibuliwa wakti wa kampeni yakiwemo mawazo ya Lipimba.
Alivishukuru vyombo vya habari kwa tendaji wao wa kazi , lakini aliviomba kufanmya kazi zaidi ya kusaidia kutibu majeraha ya nchi ili kurejesha umoja na amani badala ya kuongeza chumvi.
Dr. Mohammed Gharib Bilal - Wengi Wamerudi CCM Jee Wewe?

